• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

67 WAHITIMU CHUO CHA UKAMANDA NA UNADHIMU

67 WAHITIMU CHUO CHA UKAMANDA NA UNADHIMU Posted On: Saturday, 18th June 2022

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Stagomena Tax leo tarehe 18 Juni 2022 ametunuku Stashahada na Shahada ya Uzamili ya Mafunzo ya Ulinzi na Usalama kwa jumla ya Maafisa 67waliokua katika Chuo Cha Ukamanda na Unadhimu kilichopo Duluti Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.

Wahitimu 16 wametunukiwa Stashahada ya Mafunzo ya Ulinzi na Usalama, huku wengine 51 wakitunukiwa Shahada ya Uzamili ya Mafunzo ya Ulinzi na Usalama.

Awali, Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Brigedia Jenerali Sylivester Ghuliku aliwatunuku Wahitimu wote 67 Beji ya Ukamanda na Unadhimu Kundi la 36/21 na kuonyesha kuwa Maafisa wamemaliza Kozi hiyo yenye tija katika utendaji Kijeshi.

Akizungumza mara baada ya kutunuku Stashahada na Shahada ya Uzamili katika mafunzo ya Ulinzi na Usalama, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, amewataka Wahitimu wakaitumie elimu hiyo kutatua changamoto mbalimbali za kiusalama ikiwemo namna ya kukabiliana na matishio ya Ugaidi duniani ambayo yamekua yakisumbua kwa sasa. Pia, amesisitiza kuwa wahitimu kutoka nje wakawe mabolozi Wazuri kutokana na kila walichokipata Tanzania, na kuongeza kuwa Ulinzi na Usalama haunabudi kuimarishwa katika Jumuiya za Kikanda.

Kozi hiyo ilijumuisha Maafisa kutoka Nchi mbambali kama Bangladesh, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Misri, Eswatini, Kenya, Malawi, Msumbiji, Nigeria, Rwanda na Uganda.

Elimu walioipata Wahitimu itasaidia Majeshi ya Nchi hizo kukabiliana na changamoto za Kiulinzi, kwani kuimarika kwa Ulinzi kutasababisha Nchi kuendelea na shughuli za maendeleo na kuinua uchumi wa Nchi mbalimbali zikiwemo Jumuiya za Kikanda.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.