• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

​Buriani Waziri Kwandikwa

​Buriani Waziri Kwandikwa Posted On: Friday, 6th August 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 06 Agosti 2021 amewaongoza wananchi kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Marehemu Elias John Kwandikwa katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Aidha, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo amewaongoza Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kuuaga mwili wa Marehemu Kwandikwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.

Marehemu Waziri Kwandikwa alifariki Dunia tarehe 02 Agosti 2021 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Marehemu alizaliwa tarehe 01 Julai 1966 wilayani Kahama, mkoani Shinyanga.

Katika uhai wake marehemu Kwandikwa amewahi kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Kibaha, Mjumbe wa Kamati ya Siasa wilayani Kahama, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Shinyanga, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Mpaka umauti unamkuta alikuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Maziko yake yanatarajiwa kufanyika tarehe. 09 Agosti 2021 katika Kijiji cha Butibu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga

BWANA ALITOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.