• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Wizara ya Ulinzi na JKT yapata Waziri mpya

Wizara ya Ulinzi na JKT yapata Waziri mpya Posted On: Monday, 13th September 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri ambapo tarehe 13 Septemba, 2021 amemuapisha Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, akichukua nafasi iliyoachwa wazi baada ya aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na JKT, Hayati Elias John Kwandikwa kufariki Dunia tarehe 02 Agosti, 2021. Siku moja kabla ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Waziri wa Ulinzi na JKT, Mhe Rais alimteua Dkt. Tax kuwa Mbunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Dkt. Stergomena Tax anakuja na uzoefu mkubwa wa uongozi ikiwepo miaka minane aliyohudumu kama Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), nafasi aliyoitumikia tangu mwaka 2013.

Mawaziri wengine walioteuliwa na kuapishwa sambamba na Dkt. Tax katika viwanja vya Ikulu, Chamwino Dodoma ni pamoja na Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb) kuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. January Yusuf Makamba (Mb) kuwa Waziri wa Nishati, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb) kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi na Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mhe. Dkt. Tax anakuwa Waziri wa 17, akiwa pia Waziri wa kwanza mwanamke kuwahi kuiongoza Wizara hii tangu ianzishwe rasmi mwaka 1962.

Akiongea baada ya kuwaapisha Mawaziri hao pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samia amesema ameamua kuvunja mwiko na fikra zilizojengeka kuwa Wizara ya Ulinzi na JKT lazima iongozwe na mwanaume kwani kwa kumteua mwanamke kuwa Waziri haendi kupiga mizinga wala kushika bunduki bali Waziri anawajibika kusimamia sera na utendaji wa rasilimali watu.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.