• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Jenerali Mabeyo Ahitimisha Mafunzo

Jenerali Mabeyo Ahitimisha Mafunzo Posted On: Sunday, 26th June 2022

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Salvatory Mabeyo jana amehitimisha mafunzo ya awali ya kijeshi kwa kozi ya kuruti kundi maalum katika Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi RTS Kihangaiko iliyopo eneo la Msata mkoani Pwani.

Jenerali Mabeyo amewapongeza Askari wapya waliohitimu mafunzo hayo na kuwataka kulitumikia Taifa kwa moyo wa uzalendo na kudumisha utii, uaminifu na uhodari katika kutekeleza majukumu ya Jeshi ili nchi iendelee kuwa salama.

Sambamba na hilo amewataka Askari wapya kuilinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuulinda Uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuepuka matumizi mabaya ya mitandao, ushabiki wa kisiasa, vikundi viovu, ulevi na lugha chafu.

Aidha, Jenerali Mabeyo aliishukuru Uongozi na Wakufunzi wa RTS Kihangaiko kwa moyo wa kujituma na kuhakikisha Askari wapya wamehitimu kwa kuzingatia viwango vya mafunzo vilivyokusudiwa.

Jenerali Mabeyo pia aliwashukuru wazazi kwa kulipa Jeshi zawadi ya nguvu kazi mpya "damu changa' na hivyo wawe na moyo wa utayari watakapoona watoto wao wanapangiwa mahali popote katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya kijeshi.

Sherehe za kuhitimisha mafunzo hayo zilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo Maafisa, Askari, Wastaafu na Wazazi wa Askari wapya waliohitimu.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.