• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Jenerali Mabeyo awakaribisha nyumbani Maafisa na Askari

Jenerali Mabeyo awakaribisha nyumbani Maafisa na Askari Posted On: Monday, 15th October 2018

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Salvatory Mabeyo leo amewakaribisha nchini Maafisa na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kundi la Tano la Ulinzi wa Amani (TANZBATT-5) lililokuwa katika nchi ya Demokrasia ya Congo (DRC)na kufanya nao mazungumzo katika Chuo Maalum cha Mafunzo ya Kijeshi kilichopo Mapinga Mkoani Pwani.

Akizungumza na Maafisa na Askari waliokuwa kwenye jukumu hilo la Ulinzi wa Amani nchini humo, alisema kuwa ni furaha kubwa na ya kipekee kupata fursa ya kuwakaribisha nyumbani na hasa kwa jukumu ambalo kwa upande wetu lilikuwa ni jaribio.

Vilevile aliwapongeza kwa kazi nzuri waliyoifanya licha ya kuwa katika mazingira magumu na hatarishi kiusalama takribani kwa muda wa mwaka mzima wakati wa utekelezaji wa jukumu hilo.

Jenerali Mabeyo alitoa pole kwa mashambulizi ya kuvizia yaliyofanywa na baadhi ya vikundi vya waasi dhidi yao katika maeneo ya Simulike na Mayonga ambayo yalisababisha mauaji ya Askari 20 na wengine zaidi ya40 kujeruhiwa.

Mkuu huyo wa Majeshi alitoa pole kwa familia za wafiwa na kuwashukuru kwa moyo wa uvumilivu na subira na kuongeza kuwa ulikuwa ni msiba mkubwa si tu kwa Jeshibali ni kwa Taifa zima.

Aidha, Jenerali Mabeyo aliwaasa Maafisa na Askari wanaporudi vikosini watumie uzoefu walioupata kama somo na wawe mfano mzuri kwa wenzao. Aliendelea kwa kusema kuwa matukio yaliyotokea kamwe yasitutishe na kutukatisha tamaa bali yawe fundisho ili tuweze kubuni namna bora ya kukabiliana nayo na ikiwezekana kuzuia kabisa yasijtokeze tena.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.