• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Jenerali Mkunda ateta na Balozi wa India nchini Tanzania

Jenerali Mkunda ateta na Balozi wa India nchini Tanzania Posted On: Monday, 10th March 2025

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob John Mkunda amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India hapa nchini Mhe. Bishwadip Dey ofisini kwake Msalato Jijini Dodoma leo tarehe 10 Machi 2025.

Katika mazungumzo yao Jenerali Mkunda amempongeza Balozi Bishwadib Dey kwa kazi nzuri anayoifanya hapa nchini hususani kudumisha ushirikiano baina ya JWTZ na Jeshi la India katika nyanja ya Mafunzo, Mazoezi, na kubadilishana uzoefu wa kijeshi.

Aidha Mkuu wa Majeshi amemwomba Mhe Balozi kuendelea kudumisha ushirikiano baina ya Majeshi haya mawili ili kutoa fursa kubadilishana uzoefu katika nyanja mbalimbali za Kijeshi.

Naye Balozi Bishwadib Dey ambaye alifika Ofisini kwa Mkuu wa Majeshi kwa ziara ya kikazi, amelishukuru JWTZ kwa ushirikiano uliopo baina ya Majeshi ya nchi hizi mbili na kuahidi kuendeleza ushirikiano uliopo katika mafunzo, mazoezi na kubadilishana uzoefu wa Kijeshi.

Uhusiano uliopo baina ya Majeshi haya mawili ni muendelezo wa mahusiano ya muda mrefu baina ya Tanzania na India katika masuala ya Diplomasia ya Ulinzi.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.