• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania,latoa ufafanuzi juu ya kujiunga na mafunzo ya JKT na ajira za JWTZ

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania,latoa ufafanuzi juu ya kujiunga na mafunzo ya JKT na ajira za JWTZ Posted On: Wednesday, 7th June 2017

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),linapenda kutoa tahadhari kwa umma juu ya uwepo wa vikundi au watu wanaojifanya kuwa na uwezo wa kuwapatia vijana wa kitanzania ajira za moja kwa moja katika JWTZ au nafasi za kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa kujitolea.

JWTZ na JKT limekuwa likitoa ufafanuzi mara kwa mara wa namna ajira za JWTZ na nafasi za JKT zinavyopatikana.Usaili wa vijana wanaotaka kujiunga na JKT huanzia ngazi ya vijiji,kata, vijiji,wilaya hadi mkoa waliofaulu usaili na vipimo vya afya hupewa form za kujaza.

Pamoja na wananchi kusisitizwa kwamba hakuna gharama zozote zinazotozwa ili kupata nafasi hizo bado baadhi yao hutoa fedha kama ‘rushwa’ ili kupatiwa nafasi kinyume na taratibu zilizowekwa.kwa kukiuka taratibu zilizowekwa,wengi wamejikuta wakitapeliwa fedha zaobila kupata nafasi hizo.Baada ya kukosa nafasi hulazimika kumfuata kiongozi wa Jeshi ili kurejeshewa.

Nafasi za kujiunga na mafunzo ya JKT,hutolewa na Makao Makuu ya JKT kwa matangazo rasmi kupitia vyombo vya habari vilivyopo nchini na siyo kupitia mitandaoya kijamii wananchi wote wanatakiwa kuzingatia utaratibu huo.

Mwananchi yeyote atakayetoa fedha kwa namna yoyote ile ili kijana wake ajiunge na JKT na kisha kuwasilisha malalamiko kwamba ametapeliwa atahesabika kuwa ametoa ‘rushwa’ hivyo na

Yeye atafikishwa katika vyombo vya sheria kwa tuhuma za kutoa ‘rushwa’.Ikumbukwe kuwa, Mtoa Rushwa na Mpokea Rushwa wote ni wakosaji kwa mujibu wa sheria.

Wananchi wote mnatahadharishwa kuacha kutumia njia zisizo sahihi katika kutafuta ajira katika JWTZ au nafasi za kujiunga na JKT.Ni dhahili kuwa ukitoa fedha kwa utaratibu huo fedha yako itakuwa imepotea na nafasi hiyo hutapata.

Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.

Kwa Mawasiliano zaidi: 0756-716085

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.