• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ, Marekani wahitimisha zoezi "CUTLASS EXPRESS"

JWTZ, Marekani wahitimisha zoezi "CUTLASS EXPRESS" Posted On: Friday, 21st February 2025

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Marekani pamoja na Majeshi ya Mataifa mengine 13 wamehitimisha Zoezi la pamoja la Kijeshi la Majini "CUTLASS EXPRESS" lililolenga kuimarisha Usalama wa Majini kupitia kubadilishana Uzoefu wa kimbinu na kuboresha ujuzi wa pamoja katika kukabiliana na changamoto na Matishio ya Ulinzi na Usalama katika Bahari.

Akizungumza katika hafla ya kufunga Zoezi hilo kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Jacob John Mkunda, Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita JWTZ Meja Jenerali Ibrahim Mhona amesema lengo la Mafunzo ni namna ya kupambana na usafirishaji haramu wa binadamu, madawa ya kulevya, silaha na kupambana na Uharamia.

Aidha, Meja Jenerali Mhona amesema kupitia mazoezi hayo maafisa na Askari wa JWTZ wameweza kujengewa uwezo zaidi.

Kwa upande wake Kaimu Balozi wa Marekani nchini Mhe. Andrew Lentz amesisitiza kuwepo na ushirikiano thabiti baina ya Mataifa hayo ili kusaidia udhibiti wa matishio mbalimbali baharini.

Zoezi hilo la pamoja la Kijeshi lililokuwa likifanyika Mkoani Tanga lilifunguliwa rasmi tarehe 10 Febuari 2025 likishirikisha nchi kumi na Tano (15) ambazo ni Marekani, Ubeligiji, Comoro, Djibuti, Ufaransa, Georgia, Kenya, Madagascar, Malawi, Mauritius, Morocco, Msumbiji, Shelisheli, Somalia na Tanzania ambayo ni nchi mwenyeji.

Habari Mpya

  • JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    tokea masaa 10
  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    tokea siku 3
  • ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    tokea siku 6
  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 4
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.