• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ lajivunia Ushirikiano na Jeshi la Ujerumani

JWTZ lajivunia Ushirikiano na Jeshi la Ujerumani Posted On: Thursday, 3rd April 2025

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini Jenerali Jacob John Mkunda amekabidhiwa Rasmi Hospitali ya Daraja la Nne ya viwango vya Umoja wa Mataifa iliyojengwa kwa Ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Shirikisho la Ujerumani leo tarehe 03 Aprili 2025 Msalato Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Jenerali Mkunda ameishukuru Serikali ya Shirikisho la Ujerumani kupitia Jeshi la Nchi hiyo kwa namna linavyoshirikiana na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika nyanja mbalimbali kama vile Mafunzo, Mazoezi pamoja na Ujenzi wa Miundombinu mbalimbali ikiwemo Hospitali za JWTZ kama vile Hospitali kuu ya Jeshi Lugalo, Chuo cha Tiba cha Kijeshi na Hospitali ya Jeshi ya Kanda ya Arusha.

Aidha Jenerali Mkunda amewataka Madaktari na wauguzi watakaokuwa wakitoa huduma katika Hospitali hii kuitunza ili iendelee kutoa huduma bora kwa kizazi cha sasa na cha baadae kwani miundombinu iliyowekwa katika Hospitali hiyo ni bora na ya gharama kubwa

Naye Balozi wa Shirikisho la Ujerumani hapa Tanzania Mheshimiwa Thomas Terstegen wakati wa makabidhiano ya Hospitali hiyo,ameusifu ushirikiano mkubwa uliopo Kati ya Ujerumani na Tanzania ambapo nchi hizo zimekuwa na ushirikiano wa kindugu ambapo miradi mingi ya maendeleo imetekelezwa kwa ufanisi mkubwa.

Hospitali hiyo imejengwa katika eneo la Msalato Jijini Dodoma ambapo inatarijwa kutoa huduma za tiba kwa Maafisa, Askari na familia zao, Watumishi wa Umma pamoja na wananchi wa Dodoma na maeneo ya jirani.

Sambamba na makabidhiano ya hospitali,Serikali ya Shirikisho la Ujerumani imekakabidhi gari la kubebea wagonjwa aina ya Toyota Land Cruiser kwaajili ya matumizi ya hospitali hiyo.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.