• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ latangaza nafasi kwa Madaktari

JWTZ latangaza nafasi kwa Madaktari Posted On: Tuesday, 31st July 2018

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetangaza nafasi kwa wataalamu wa Tiba watakaotoa huduma za afya katika hospitali, vituo vya afya na zahanati za Jeshi hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, msemaji wa JWTZ Kanali Ramadhani Dogoli amesema, JWTZ limetoa nafasi ya kuandikishwa Jeshini kwa watanzania wenye taaluma zifuatazo:- Doctor of Medicine, Doctor of Dental Surgery, Bachelor of Pharmacy, BSC in Health System Management, Bachelor in Laboratory Science, Bachelor of Science in Nursing, Bachelor of Science in Physiotherapy na Bachelor of Science in Prosthetics and Orthotics.

Akifafanua zaidi Kanali Dogoli amesema, walengwa watakaoandikishwa Jeshini ni wale wenye sifa zifuatazo;-

a.Awe raia wa Tanzania kwa kuzaliwa,

b.Awe na umri kati ya miaka 18 na 28,

c.Awe na afya njema ya mwili na akili,

d.Awe mwenye tabia njema na nidhamu nzuri na

e.Awe hajawahi kupatikana na hatia ya makosa ya jinai Mahakamani na kufungwa jela

Pamoja na sifa hizo atakayependa kuandikishwa jeshini pia anatakiwa awe na;-

a. Cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate),

b.Vyeti vya shule (Academic & School Leaving Certificates) na

c.Vyeti vya Chuo (Transcript & Academic Certificates).

Aidha, Kanali Ramadhani Dogoli aliongeza kuwa, Daktari anatakiwa awe amemaliza mafunzo kwa vitendo (Internship) na kutunukiwa vyeti pamoja na kusajiliwa na Bodi. Vilevile anayehitaji anatakiwa awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo.

Kanali Ramadhani Dogoli amewataka wenye sifa hizo na wanaohitaji kujiunga na JWTZ waripoti katika Kambi ya Jenerali Abdallah Twalipo, Mgulani jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti 2018 kuanzia saa 1.00 Asubuhi kwa ajili ya usaili.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.