• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ limeaga miili ya marehemu Koplo Marcelino Pascal Fubusa na Praiveti Venance Moses Chiboni

JWTZ limeaga miili ya marehemu Koplo Marcelino Pascal Fubusa na Praiveti Venance Moses Chiboni Posted On: Monday, 16th October 2017

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeaga miili ya marehemu Koplo Marcelino Pascal Fubusa na Praiveti Venance Moses Chiboni, leo tarehe 16 Octoba 2017 katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali James Mwakibolwa, Makamanda na Wanadhimu mbalimbali wa JWTZ pamoja na ndugu, jamaa na marafiki waliaga kwa huzuni miili ya marehemu hao.

Akizungumza wakati wa kuaga marehemu, Waziri wa Ulinzi na JKT amewataka maafisa na askari kutokata tamaa isipokuwa tukio hilo liwape nguvu na ushupavu katika kutekeleza majukumu yao.

Marehemu hao waliuawa wakiwa katika jukumu la Ulinzi wa Amani nchini DRC baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi na kundi la waasi tukio ambalo lilitokea tarehe 09 Octoba 2017 umbali wa kilomita 24 mashariki mwa mji wa Beni.

Baada ya tukio hilo la kushtukizwa, Majeshi yetu yalifanikiwa kuwarudisha nyuma waasi hao na kudhibiti eneo hilo.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.