• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ watakiwa kufanya kazi kwa Weledi

JWTZ watakiwa kufanya kazi kwa Weledi Posted On: Friday, 22nd December 2023

Mkuu wa Tawi la Ugavi na Uhandisi wa JWTZ Meja Jenerali Hawa Kodi amewataka Wataalam wa Lojistiki ndani ya JWTZ kuwa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yao wakati wa Amani na wakati wa vita ili kuviwezesha vikosi wanavyovihudumia kufanya majukumu yao bila changamoto zozote pindi wanapokuwa kwenye majukumu ya kioperesheni na kwenye mazoezi ya medani.

Meja Jenerali Kodi ameyasema hayo wakati akifunga semina ya wataalam wa Lojistiki iliyofanyika katika Shule ya Mafunzo ya Huduma Pangawe Mkoani Morogoro.

Amesisitiza kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda anaendelea kulijengea uwezo JWTZ kwa zana, mitambo na vifaa mbalimbali vya kisasa vinavyorahisisha utendaji kazi pindi wanapopewa majukumu ya kuvihudumia vikundi vinapokuwa katika operesheni mbalimbali hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi na ufanisi mkubwa.

Nae Mkuu wa Shule ya Huduma Pangawe Brigedia Jenerali Pasian Chausi amesema kuwa semina imeandaliwa kwa nia ya kuwajengea uwezo washiriki ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia na matishio yanayoikabili Dunia kwa wakati huu.

Semina hiyo iliyofunguliwa na Mkuu wa Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo Meja Jenerali Dkt. Gabriel Muhidze imefanyika kwa muda wa wiki mbili kuanzia tarehe 11 Desemba hadi tarehe 22 Desemba mwaka huu.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.