• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ yaanza kutoa huduma ya matibabu ya Figo

JWTZ yaanza kutoa huduma ya matibabu ya Figo Posted On: Wednesday, 23rd October 2019

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt.Hussein Mwinyi (MB) leo tarehe 23 Oktoba 2019 amefungua rasmi kitengo kipya cha matibabu cha kusafisha figo (Dialysis) katika Hospitali Kuu ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Katika ufunguzi huo Mhe. Waziri alitoa shukrani zake za dhati kwa Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Jeshi katika kuboresha utoaji wa huduma ya afya nchini.

Aidha, Waziri Mwinyi alimpongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange (mstaafu) kwa kuanzisha wazo hilo na kuungwa mkono na wasaidizi wake akiwemo Mkuu wa Majeshi wa sasa Jenerali Venance Mabeyo kwa kuliendeleza wazo hilo mpaka kufikia hatua hii ya kuanza kutoa huduma ya matibabu ya kusafisa figo.

“Kufunguliwa kwa jengo na utoaji wa huduma hii katika Hospitali ya Jeshi, itapunguza gharama kwa Jeshi kwani Maafisa, Askari, familia zao na watu wengine wataipata huduma hii hapahapa nchini na kwa bei nafuu zaidi na hivyo kuweza kuokoa maisha ya watanzania walio wengi ambao walikuwa wanashindwa kuwapeleka ndugu zao nje ya nchi”.

Kwa upande wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo aliwataka wataalamu wa kitengo hicho kuwa makini katika utendaji wa kazi kwani suala la tiba ya figo linahitaji umakini mkubwa. Kwamujibu wa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Jeshi Lugalo Brigedia Jenerali Gabriel Mhidzealisema kitengo hicho kipya cha usafishaji wa figo kinauwezo wa kuhudumiawagonjwa wa figowasiopungua 40 kwa siku, ambapo katika mashine kumi zilizofungwa katika kitengo hicho kila mashine inauwezo wa kuhudumia wagonjwa wasiopungua watano (5).

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.