• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ YAKABIDHI KIJITI KWA ZIMBABWE

JWTZ YAKABIDHI KIJITI KWA ZIMBABWE Posted On: Thursday, 14th March 2024

Nchi ya Zimbabwe leo imekabidhiwa Uenyekiti wa Kikundi Kazi cha Rasilimali Watu cha Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Arusha baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kikundi Kazi hicho Meja Jenerali Marco Gaguti kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kumaliza muda wake.

Meja Jenerali William Dube kutoka nchini Zimbabwe ndiye anayechukua nafasi hiyo kwa sasa.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa kijiti hicho cha Uongozi, Meja Jenerali William Dube ameipongeza Tanzania kupitia JWTZ kwa kuweza kutekeleza majukumu yake kwa weledi na hivyo kufanikisha kukamilika kwa kazi ya kuandaa taratibu za kiutendaji zitakazotumika na Jumuiya hiyo katika majukumu yake ya ulinzi wa amani yanayoendelea nchini Msumbiji na DRC.

Aidha, Meja Jenerali William Dube amesema kuwa kupitia Jumuiya hiyo nchi wanachama wa SADC zitakuwa sehemu salama kwa kuishi bila migogoro na hivyo kuwawezesha wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Nae Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Meja Jenerali Marco Gaguti kutoka JWTZ, amewashukuru wajumbe wote wa Kikundi Kazi cha Rasilimali Watu cha Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika kwa ushirikiano waliompa wakati wote wa uongozi wake na kufanikisha kukamilisha jukumu alilopewa kwa weledi.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.