• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda Posted On: Saturday, 5th July 2025

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania limetoa msaada wa maboksi mia moja ya vigae na matenki matano yenye ujazo wa lita elfu kumi kila moja kama mchango wake katika ujenzi wa nyumba nane zilizopo Wilaya ya Karongi nchini Rwanda, kwaajili ya manusura wa mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda,Mkurugenzi wa Tiba wa JWTZ Brigedia Charles Emilio Mwanziva amesema kuwa pamoja na kukabidhi vifaa hivyo,pia JWTZ limetoa wataalam wa Tiba ambao wameungana na wengine kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kushiriki kutoa huduma kwenye hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini humo ikiwa ni sehemu ya mpango wa Majeshi ya Jumuiya kuimarisha uhusiano wao na wananchi kwenye nchi wanachama.

Naye Meya wa Mji wa Karongi Mheshimiwa Kazungu amelishukuru JWTZ kwa msaada lililoutoa huku akiainisha kuwa mpango wa kuwapatia makazi bora manusura hao unafanyika nchi nzima kwa kuzingatia matumizi bora ya ardhi ili kuhakikisha wananchi wanapata maeneo kwaajili ya shughuli za Kilimo huku Serikali ikitenga maeneo ya uwekezaji ili kukuza uchumi wa Taifa hilo.

Amesifu mpango wa Majeshi ya EAC katika kuhakikisha kuwa yanashiriki shughuli za kimaendeleo kwani kwa kufanya hivyo yanawafanya wananchi kuwa karibu nayo na kutoa ushirikiano mkubwa pindi wanapowahitaji.

Tukio la kukabidhi misaada hiyo limefuatiwa na uzinduzi nyumba hizo ambapo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchi anayehusika na Serikali za Mitaa Nchini Rwanda Mheshimiwa Maria Sorange Kaisire

EAST AFRICA CIVIL MILITARY COOPERATION ACTIVITIES ni mpango uliobuniwa na Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii na kujenga mahusiano mazuri kati ya Majeshi na raia ambapo hii ni mara ya tano shughuli hizo kufanyika ambapo hufanywa kwa mzuguko ndani ya nchi wanachama.

Habari Mpya

  • JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    tokea masaa 12
  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    tokea siku 3
  • ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    ​MEJA JENERALI GAGUTI AHITIMISHA MAFUNZO ASKARI WAPYA.

    tokea siku 6
  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 4
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.