• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Kamati ya Bunge yakagua Ujenzi Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa

Kamati ya Bunge yakagua Ujenzi Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Posted On: Wednesday, 12th March 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imefanya ziara kutembelea ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, Dodoma leo tarehe 12 Machi 2025 na kupongeza mafanikio yaliyofikiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Namtumbo Mheshimiwa Vita Kawawa amempongeza Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salum Haji Othman kwa mafanikio makubwa ya ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa.

Kamati hiyo imelipongeza JWTZ kwa kukidhi vigezo vya ujenzi, ubora wa jengo na imeahidi kuendeleza ushirikiano ili kufikia lengo lililokusudiwa.

Kwa upande wake Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salum Haji Othman ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa kwani ni mafanikio makubwa kwa JWTZ kuwa na Makao Makuu ya Jeshi yaliyojengwa kwa kiwango cha Kimataifa.

Aidha, baada ya kukagua maeneo mbalimbali ya ujenzi ikiwemo ofisi za Wizara ya Ulinzi na JKT, Kamati hiyo ilitembelea ujenzi wa hospitali Kuu ya Jeshi ya ngazi nne, inayoendelea kujengwa eneo la Msalato, Dodoma.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.