• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya ZNZ yafana

Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya ZNZ yafana Posted On: Sunday, 12th January 2020

Sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar yamefanyika Januari 12, 2020 katika Uwanja wa Aman, Zanzibar.

Maadhimisho hayo yaliongozwa na Rais na Mwenyekiti wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali wakiwemo wastaafu.

Baadhi ya viongozi hao ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa.

Wengine ni Marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa, Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Aman Abeid Karume.

Akihutubia wananchi waliohudhuria kwenye maadhimisho hayo, Rais Dkt. Shein alisema Serikali anayoiongoza itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kikatiba na kisheria katika kulinda amani, utulivu na maisha ya wananchi na mali zao.

Aliendelea kusema kuwa suala la kudumisha amani halina mbadala na kusisitiza kuwa Serikali haitosita kumchukulia hatua mtu yeyote atakaejaribu kuhatarisha amani ya nchi.

Aidha, Maadhimisho hayo yalipambwa na vitendo vya kijasiri vilivyoonyeshwa na makomando kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania .

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.