• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Mafunzo Maalum ya Kupambana na Vitendo vya Uhalifu Duniani Yahitimishwa

Mafunzo Maalum ya Kupambana na Vitendo vya Uhalifu Duniani Yahitimishwa Posted On: Saturday, 11th September 2021

Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita wa Kamandi ya Vikosi chini ya Makao Makuu ya Jeshi Brigedia Jenerali Iddi Nkambi amehitimisha rasmi mafunzo maalum ya kupambana na vitendo vya uhalifu vinavyojitokeza kwenye mataifa mbalimbali duniani.

Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Kunduchi Dar es salaam, yametolewa kwa askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wale wa Jeshi la Marekeni, Kamandi ya Afrika.

Akizungumza mara baada ya kuhitimisha mafunzo hayo, Brigedia Jenerali Nkambi amesema mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuunganisha nguvu kati ya Tanzania na Marekani katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu wa kimataifa, ikiwemo ugaidi vinavyotishia ulimwengu kwa sasa.

Kwa upande wake Kaimu Kamanda kikosi maalum cha JWTZ, Luteni Kanali Cliff Kulya amesema mafunzo hayo yamehusisha maafisa na askari wenye taaluma maalum na yametoa fursa kujifunza kwa pande zote mbili namna ya kukabiliana na uhalifu usiojali mipaka ya nchi.

Wakati huo huo, mwakilishi kutoka Marekani Kapteni Matt Gooh amesema mafunzo yalikuwa mazuri na yenye tija. Akaongeza kuwa "ni vyema pande zote kutumia ipasavyo uzoefu waliobadilishana katika mafunzo hayo".

Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi julai 28, 2021 na Mkuu wa Kamandi ya Afrikawa Jeshi la Marekani, Jenerali Stephen Townsend na kuhitimishwa Septemba 10, 2021.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.