• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Magdalena Shauri awaduwaza Wakenya

Magdalena Shauri awaduwaza Wakenya Posted On: Tuesday, 20th August 2019

Ama kweli Kutangulia siyo kufika na Riziki ya Mja haipotei bali huja kwa wakati autakao Mola, kauli hizi zilijidhihirisha pale Mwanariadha wa TanzaniaMagdalena Crispin Shauri alipowashangaza wengi na kutoamini kile kilichokuwa kikitokea kwa watu waliofurika kushuhudia Mbio za Nyika (10 Km) katika Viwanja vya Kambi ya Jeshi la Nchi Kavu(Kahawa Barracks) hapa Nairobi nchini Kenya alipotoka nyuma na kumpita Mkenya Perine Nenkampi aliyekuwa akiongoza mbio hizo na kufanikiwa kumpita meta10 kabla ya kumaliza mbio hizo

Kitendo hicho kiliibua shangwe siyo tu kwa Watanzania bali hata kwa wale ambao waliokuwa wakifuatilia mpambano huo mkali baina ya wawili hao. .

Katika mchezo huo uliogawanyika katika makundi mawili yaani Wanaume na Wanawake Magdalena Crispin Shauri aliyemaliza nafasi ya kwanza kwa kutumia 33:09:22, na kupata medali ya Dhahabu, akifuatiwa na Mkenya Perine Nenkampi 33:12:07 (Silver) na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Doreen Chesang waKenya 33:23:02 aliyepata Bronze

Kwa upande wa Wanaume, Mkenya Kibinot Kandie alishika nafasi ya Kwanza kwa kutumia 28:42:05 alipata Medali ya Dhahabu huku akifuatiwa na Mkenya Phenus Kipleting aliyetumia 28:49:02, nafasi ya tatu ilichukuliwa na Isaac Kibet kutoka Uganda kwa kutumia 28:55:00.

Mchezo huo ulianza majira ya saa Tatu asubuhi na kufunguliwa rasmi na Makamu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini Kenya Luteni Jenerali Robert Kibochi uliwavutia watu wengi.

Viongozi mbalimbali wa Majeshi na wengine kutoka katika Jumuiya Afrika Mashariki walihudhiria wakati wa Mchezo huo. Miongoni wa wageni hao ni Makamu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Burundi Meja Jenerali Joseph Ndayishimiye,Mkuu wa Msafara wa Tanzania Meja Jenerali Othman Sharif, Mwenyekiti wa Maandalizi ya Michezo ya Majeshi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki Meja Jenerali Ferdinand Safari, Mkuu wa Msafara wa Uganda Brigedia Jenerali Francis Takirwa, Mkuu wa Msafara wa Rwanda Brigedia Jenerali Emmanuel Bayinganana Mkuu wa Msafara wa Burundi Kanali Jean Habarugira na wengine.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.