• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Mama Samia: Rais wa Kwanza Mwanamke Tanzania

Mama Samia: Rais wa Kwanza Mwanamke Tanzania Posted On: Friday, 19th March 2021

Mama Samia Suluhu Hassan ameapishwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibrahim Hamis Juma leo Machi 19, 2021 kuwa Rais wa Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama hitajio la Kikatiba kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Tukio hilo limefanyika Ikulu ya Magogoni jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Rais wa Nane wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Marais wastaafu wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Mara baada ya kuapishwa Rais Samia Suluhu Hassan alipigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride maalum lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuonesha kumtambua na kumtii kama Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania.

Aidha, mtangulizi wake, Hayati Rais John Pombe Magufuli aliaga dunia Jumatano Machi 17, 2021 kwa ugonjwa.

Hatua hiyo ni utekelezaji wa Kifungu cha 37 (5) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa madarakani hadi mwaka 2025 wakati wa uchaguzi mwingine mkuu wa Rais na atakua na haki ya kugombea kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Mama Samia anakuwa Mwanamke wa kwanza kuwa Rais nchini na Afrika Mashariki.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.