• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi la mchezo wa Gofu "CDF Golf Trophy 2022" yafungwa

Mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi la mchezo wa Gofu "CDF Golf Trophy 2022" yafungwa Posted On: Monday, 3rd October 2022

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amefunga rasmi mashindano ya Kombe la Mkuu wa Majeshi la mchezo wa Gofu "CDF Golf Trophy 2022" katika viwanja vya Gofu Lugalo Jijini Dar es Salaam na kutoa zawadi mbalimbali kwa washindi wa mchezo huo.

Mashindano hayo yalihusisha vilabu mbalimbali vya mchezo wa Gofu hapa nchini pamoja na Klabu ya Gofu kutoka Lilongwe nchini Malawi ikiongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Malawi Jenerali Vincent Nundwe aliyeambatana na Maafisa Jenerali kutoka nchini humo.

Awali ya yote Mwenyekiti wa klabu ya mchezo wa Gofu Lugalo, Brigedia Jenerali Michael Luhongo (Mstaafu) alimkaribisha mgeni maalum Mkuu wa Majeshi ya Malawi Jenerali Vincent Nundwe ambaye alitoa zawadi kwa Jenerali Jacob Mkunda na kumpongeza Kwa kuteuliwa kwake kuwa mlezi mpya wa Klabu ya Gofu Lugalo, nafasi ambayo alikabidhiwa na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu),

Jenerali Nundwe pia alipata fursa ya kutoa zawadi kwa Jenerali George Waitara (mstaafu), Meja Jenerali Said Mkambi na Brigedia Jenerali Michael Luhongo (mstaafu) kwa kuuendeleza na kujenga hamasa ya mchezo huo ambapo alisema kuwa mchezo wa gofu unajenga umoja na kuimarisha undugu kitaifa na kimataifa.

Jenerali Nundwe ameialika Klabu ya mchezo wa gofu Lugalo kwenda nchini Malawi mwezi Novemba mwaka huu kwa ajili ya kushiriki mchezo wa golf nchini humo.

Sambamba na hilo mwakilishi wa Benki ya NMB ndugu Philbert Mponzi alimshukuru Jenerali Mkunda kwa kuendeleza mchezo wa Golf na kuahidi kuwa Benki ya NMB itaendelea kuwa miongoni mwa wadhamini wa mchezo huo.

Jenerali Jacob Mkunda alihitimisha shughuli hiyo kwa kumshukuru Mkuu wa Majeshi ya Malawi Jenerali Vincent Nundwe, Maafisa na Wadhamini, Wachezaji na Wadau wa mchezo huo kwa kuboresha na kuuendeleza klabu ya mchezo wa gofu Lugalo

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.