• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Kikao cha Kamati ya utendaji ya Ulinzi na usalama ya Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika (SADC)

Kikao cha Kamati ya utendaji ya Ulinzi na usalama ya Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika (SADC) Posted On: Monday, 22nd May 2017

Kamati ya utendaji ya ulinzi na usalama ya Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika (SADC) imekutana na kufanya kikao kuanzia tarehe 15-19 Mei 2017 jijini Dar es salaam.Kikao hicho kimehudhuriwa na Wakuu wa Majeshi wa nchi wanachama pamoja na wawakilishi wa Wakuu wa Majeshi kwa nchi ambazo Wakuu wa Majeshi hawakuweza kuhudhuria kutokana na sababu mbalimbali. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho.

Hata hivyo, kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha kamati ndogo ya utendaji ya Ulinzi na Usalama kilicho funguliwa na Mkuu wa mafunzo na utendaji kivita wa JWTZ Meja Jenerali Issa Nassor Mei 15 na kufungwa Mei 17 mwaka huu.Baadaye kikao kiliendelea na kuongozwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania.

Baadhi ya mambo yaliyo jadiliwa ni pamoja na hali ya Ulinzi na Usalama kwa nchi wanachama, Afrika na duaniani kwa ujumla.Vilevile masuala ya Ulinzi wa Amani katika Afrika hususani kwa wanachama wa SADC pia yalijadiliwa.

Aidha, utekelezaji wa Maazimio mbalimbali ya jumuiya hiyo yaliweza kujadiliwa wakati wa kikao hicho. Vilevile mpango kazi wa Jumuiya hiyo uliwekwa wazi ili nchi wanachama waweze kujiandaa kuutekeleza ikiwa ni pamoja na kutekeleza majukumu ya msingi ya jumuiya hiyo kwa muda uliopangwa.

Aidha, kikao kama hicho hufanyika kila mwaka kwa mzunguko kwa nchi mwanachama.Nchi mwenyeji hutoa mwenyekiti wa kikao.Mwaka huu Tanzania ilikuwa mwenyeji.


Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.