• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda Posted On: Monday, 28th April 2025

Mkuu wa Kamandi ya Vikosi Chini ya Makao Makuu ya Jeshi Meja Jenerali Iddi Nkambi kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi John Mkunda amekutana na Kufanya mazungumzo na Mkuu wa Jeshi la Akiba Kutoka Nchini Uganda Meja Jenerali Willium Don Nabasa pamoja na timu yake katika ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi ya zamani yaliyopo Upanga Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo Meja Jenerali Nkambi amesema Tanzania na Uganda ni nchi zenye historia kubwa katika masuala mbalimbali ya ushirikiano toka enzi za uongozi wa Hayati Mwalimu Nyerere, hivyo kuja kwao nchini ni sehemu moja wapo ya kujifunza masuala mbalimbali ya utendaji ndani ya Jeshi la akiba pamoja na kuendelea kushirikiana kutatua changamoto mbalimbali za kiutendeji kwa lengo la kuongeza ufanisi na kuweza kupiga hatua zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Akiba kutoka nchini Uganda Meja Jenerali Nabasa, amelishukuru Jeshi la wananchi wa Tanzania pamoja na serikali kwa ujumla kwa kuendelea kushirikiana nao huku akisema wamekuja nchini kwa lengo la Kujifunza masuala mbalimbali ya utendaji yanayohusu Jeshi la Akiba.

Mkuu huyo wa Jeshi la akiba pamoja na timu yake kutoka nchini Uganda wapo nchini kwa ziara maalumu kwa lengo la kuona, kujifunza na kujadiliana na mwenyeji wake Mkuu wa Jeshi la akiba nchini Brigedia Jenerali Erick Mlelwa masuala mbalimbali yanayohusiana na Jeshi la akiba nchini.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.