• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

​Mnadhimu Mkuu wa JWTZ atembelea mradi wa kilimo cha Mpunga Chita

​Mnadhimu Mkuu wa JWTZ atembelea mradi wa kilimo cha Mpunga Chita Posted On: Friday, 12th February 2021

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Yacoub Mohamed amefanya ziara ya kikazi na kutembelea mradi mkubwa wa kimkakati wa kilimo cha Mpunga katika kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa Chita, Wilayani Kilombero mkoani Morogoro tarehe 12 Februari 2021. Mradi huo unaogharimu shilingi Bilioni nne za kitanzania ni mkakati wa makusudi wa kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua.

Aidha, mradi huo ukikamilika unategemewa kuwa na jumla ya ekari 12000 ambapo hadi sasa ekari 2500 zimeshalimwa mpunga. Mradi huo utakuwa ndio mradi mkubwa hapa nchini wa kilimo cha Mpunga kwa njia ya umwagiliaji wenye lengo la kuongeza uzalishaji wa mchele nchini.

Luteni Jenerali Mohamed alilipongeza Jeshi la Kujenga Taifa kwa kubuni mradi huo wenye lengo la kuliletea Jeshi na Taifa tija zaidi.

Akiongea na Maafisa na Askari wa Kikosi hicho, Mnadhimu Mkuu alisisitiza nidhamu na weledi kazini na kudumisha ushirikiano uliopo wa vyombo vya Ulinzi na Usalama katika kulinda Taifa.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.