• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

NETBALL TANZANIA YAENDELEZA USHINDI

             NETBALL TANZANIA YAENDELEZA USHINDI Posted On: Saturday, 17th August 2019

Timu ya Mpira wa Pete ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) leo tarehe 17 August 2019 imeendeleza wimbi la ushindi katika Mashindano ya Majeshi yanayoendelea Nchini Kenya baada ya leo kuifunga timu ya Jeshi la Burundi kwa jumla ya magoli 99-16.

Katika mchezo uliopigwa katika Uwanja waShule ya Fedha hapa mjini Nairobi, Tanzania ilionesha kuwamudu vema wapinzani wao toka kipindi cha robo ya kwanzabaada ya kuwafunga magoli 38-4.

Aidha, katika robo ya pili Tanzania ikiongozwa na mfungaji wake mahili Koplo Mwanaidi Hassan iliongeza wimbi la magoli nampaka wanakwenda mapumziko Tanzania ilikuwa ikiongoza kwa jumla ya magoli 49-7.

Huu ni mchezo wake wa pili kwa Timu hiyo, na imefanya vizuri katika michezo yake yote. Katika mchezo wa kwanza iliweza kuifunga Timu Jeshi la Rwanda kwa jumla ya magoli 66-16.

Mwaka huu katika mashindano haya jumla ya nchi Wanachama sita zimeshiriki ikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Sudan Kusini na kuna jumla ya michezo mitano itashindaniwa ikiwa ni Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Kikapu, Mpira wa Wavu na Riadha.

Mara ya mwisho mashindano haya yalifanyika nchini Burundi na Tanzania ilinyakua nafasi ya kwanza katika mchezo huu wa Mpira wa Pete.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.