• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Rais Magufuli atembelea Kikosi cha Usafirishaji cha JWTZ

Rais Magufuli atembelea Kikosi cha  Usafirishaji cha JWTZ Posted On: Saturday, 10th November 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli leo Novemba 11 amefanya ziara fupi katika kikosi cha Usafishaji cha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kilichopo jijini Dar es salaam na kujionea utayari wa kikosi hicho katika kutekeleza majukumu yake kijeshi na kitaifa pindi itakavyohitajika.

Rais Magufuli akiwa kikosini hapo alipata fursa ya kutembelea magari yenye uwezo wa kubeba uzito tofauti yanayotumika katika kutekeleza majukumu yake.

Aidha aliliagiza Jeshi liwe tayari katika zoezi aliloliita "Operesheni Korosho" linalotarajiwa kufanyika katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga na Pwani.

Alisema " zoezi hilo litafanyika endapo agizo la Serikali la kuwataka wanunuzi wa Korosho kununua zao hilo kwa muda uliopendekezwa kushindikana.

Rais Magufuli alilipongeza Jeshi kwa kuwa mfano mzuri kwa Majeshi mengine Barani Afrika kwa utendaji kazi wake na kuwa na historia nzuri ya kupigania uhuru wa Bara la Afrika na kuwa historia hiyo haitafutika kamwe.

Vile vile alisisitiza umuhimu wa Serikali kuzidi kuliongezea nguvu JWTZ katika nyanja ya usafirishaji.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.