• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

TANZANIA YAENDELEZA UBABE KWA KENYA

                              TANZANIA YAENDELEZA UBABE KWA KENYA Posted On: Tuesday, 20th August 2019

Takribani ni mwezi mmoja umepita sasa toka Timu ya Taifa ya Tanzania “Taifa Stars” imeitoa Harambee Stars kwenye Michuano ya kuwania kufuzu kwenye Mashindano ya CHAN. kwa mikwaju ya Penati.

Tarehe 13 Agosti mwaka huu Michezo ya Majeshi kwa nchi za Afrika Mashariki yalizinduliwa rasmi na Waziri wa Ulinzi wa Kenya Balozi Raychelle Omamo kwa kuwataka washiriki kutambua kuwa michezo hiyo inalengo la kuwafanya Wanaafrika Mashariki kuendeleza hali ya Amani na utulivu iliyopo baina nchi wanachama kwa kupitia michezo.

Katika mwendelezo wa michezo hiyo leo tarehe 19 Agosti 2019, Tanzania ikiwakilishwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linashiriki kwa kupeleka timu tano za michezo tofauti. limeweza kushiriki katika michezo mitatu.

Katika mchezo wa Mpira wa miguu Tanzania imeweza kuwafunga wenyeji Ulinzi Stars2-1. Mchezo ulionza katika majira ya saa kumi na nusu Tanzania walikuwa wa kwanza kuliona lango la Ulinzi Stars, katika dakika (08) lililofungwa na kiungo wake machachali Kelvin Nashoni baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Samweli Kamuntu na kuachia shuti kali lilikwenda nyavunimoja kwa moja.

Kipindi cha pili Kenya walifanya mabadiliko kwa kumwingiza Enosi Ochieng, mabadiliko hayo m yaliweza kuwasaidiana kupata goli katika dakika (53). Tanzania nao walifanya mabadilikokatika dakika (58) kwa kuwatoa Prosper Nkwama na kumwingiza Najim Magulu, Mgandila Shabani/Hassan Gumbo na Samwel Kamuntu alimpisha Hussein Nyamanduru (Agogo). Mabadilko hayo yaliendelea kuwaweka pabaya wenyeji kwani mnamo dakika ya (74) ya mchezo Nahodha wa wa Timu ya Tanzania Fuluzulu Maganga aliweza kuipatia timu yake bao la pili na la ushindi na kuwaacha wenyeji wakiduwaa wasijue la kufanya.

Mgeni rasmi katika mchezo huo alikuwa Waziri wa Ulinzi wa Kenya Balozi Raychelle Omamo aliyeambatana na Makamu Mkuu wa Majeshi ya Kenya Luteni Jenerali Robert Kibochi, Meja Jenerali (wa kwanza nchini Kenya) Fatuma Mohammed, Mkurugenzi wa Michezo JWTZ Kanali Erasmus Bwegoge na viongozi wengine.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.