• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

TANZIA

TANZIA Posted On: Monday, 15th February 2021

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo anasikitika kutangaza kifo cha Afisa Mkuu Brigedia Jenerali Francis Xaiver Mbenna (Mstaafu), kilichotokea tarehe 13 Februari, 2021 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo.

Marehemu alizaliwa tarehe 31 Julai, 1930 katika Kijiji cha Nakayaya, Kata ya Mlingoti, Tarafa ya Mlingoti, Wilaya ya Tunduru katika Mkoa wa Ruvuma. Alipata Elimu katika ngazi mbalimbali ikiwemo Stashahada ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Hull nchini Uingereza mwaka 1960 hadi mwaka 1961.

Marehemu alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mwaka 1974. Alihudhuria kozi ya Afisa Mwanafunzi hapa nchini mwaka 1974 na kutunukiwa Kamisheni tarehe 01 Julai, 1975. Marehemu alipanda vyeo ngazi kwa ngazi hadi cheo cha Brigedia Jenerali tarehe 30 Machi, 1987. Marehemu alitumikia Taifa kwa muda wa miaka 34, miezi 6 na siku moja (1) hadi alipostaafu utumishi Jeshini kwa umri tarehe 30 Juni, 1988.

Brigedia Jenerali Francis Xaiver Mbenna (Mstaafu) alitunukiwa Medali mbalimbali wakati wa utumishi wake ifuatavyo:- Medali ya Vita; Miaka 20 ya JWTZ; Utumishi Mrefu Tanzania na Utumishi Uliotukuka Tanzania.

Katika utumishi wake, Marehemu aliwahi kushika madaraka mbalimbali yakiwemo Mwalimu Mkuu Songea Boys mwaka 1960 hadi 1964; Mkurugenzi wa Mafunzo na Elimu Jeshini mwaka 1985 hadi 1988 na Makamu Mwenyekiti Taifa, Chama cha Wazee (SAWATA) kuanzia mwaka 1999 hadi mwaka 2005.

Heshima za mwisho kwa marehemu zitatolewa Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo tarehe 16 Februari, 2021 kuanzia saa 3:00 asubuhi na kuzikwa siku hiyo hiyo katika makaburi ya Temeke Wailes jijini Dar es Salaam saa 9:00 alasiri. Marehemu ameacha mke na watoto.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.