• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Washiriki Zoezi Ushirikiano Imara 2022 Wakabidhiwa Bendera

Washiriki  Zoezi Ushirikiano Imara 2022 Wakabidhiwa Bendera Posted On: Tuesday, 24th May 2022

Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la nchi Kavu Meja Jenerali Anthony Chacha Sibuti leo tarehe 24 may,2022 kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi amekabidhi bendera ya Taifa kwa kikundi kinachokwenda kushiriki zoezi la Ushirikiano Imara 2022 la Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mji wa Jinja nchini Uganda. Luteni Kanali Lucas Wambura Ryoba kamanda kikosi cha Tanzania alipokea kuashiria kwamba kikundi kipo tayari kuiwakilisha nchi katika zoezi hilo.

Zoezi la Ushirikiano Imara ni zoezi la Kijeshi lililoandaliwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka Majeshi ya Ulinzi, Polisi na mamlaka za kiraia (military, police & civilian component) ambapo washiriki watajikita katika maeneo manne (4) muhimu ambayo ni operesheni za ulinzi wa Amani, kukabiliana na maafa/majanga, kupambana na uharamia na kupambanana ugaidi.

Aidha zoezi hili ni la kumi na mbili (12) tangu kuanzishwa kwa mazoezi haya mwaka 2011 na washiriki kutoka Tanzania ni JWTZ, Polisi, Magereza, Zimamoto na uokoaji, Uhamiaji, Wizara ya Mambo ya Nje, Ofisi ya Rais na Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha maafa na kituo cha kitaifa cha kupambana na Ugaidi. Lengo kuu ni kuzijengea nchi wanachama wa jumuiya katika kukabiliana na changamoto za kiusalama kwa pamoja na kudumisha ushirikiano baina ya vyombo vya Ulinzi na Usalama na wadau wengine katika operesheni za ulinzi wa Amani.

Pamoja na hayo Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu aliwaasa washiriki wa zoezi kuwa na ushirikiano miongoni mwao kama watanzania na nchi zingine na kusistiza wajifunze mambo mazuri kutoka kwa nchi zingine bila kusahau kudumisha nidhamu ,uhodari na utendaji mzuri.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.