• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri Jafo afungua Kozi Fupi ya Viongozi

Waziri Jafo afungua Kozi Fupi ya Viongozi Posted On: Monday, 29th July 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mheshimiwa Selemani Said Jafo leo amefungua Kozi Fupi Kundi la Saba ya Viongozi inayoendeshwa katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) kilichopo Kunduchi jijini Dar es Salaam kinachomilikiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Akifungua Kozi hiyo Waziri Jafo alisema kuwa washiriki hao wanatakiwa kuifanyia kazi kaulimbiu ya “Uzalendo na Utaifa ni Nguzo za Usalama wa Nchi” pindi watakaporudi katika vituo vyao vya kazi ili kurekebisha tabia za baadhi ya Watendaji ambao wamekuwa wakitoa taarifa za siri kwa watu wasiohusika na kuleta sintofahamu baina ya Serikali na Wananchi na hivyo kupelekea uvunjifu wa Amani nchini.

Aidha, alisisitiza kuwa ili nchi iweze kufikia Uchumi wa Kati suala la usalama ni lazima lipewe kipaumbele kwa kila mmoja wetu.

“Hatuwezi kufikia Uchumi wa Kati kama usalama wa Nchi upo mashakani na kuhisi kuwa susla hilo ni la Vyombo vya Ulinzi na Usalama peke yao, kwani tumeshuhudia mataifa mengi yakiporomoka kiuchumi kutokana na ukosefu wa Usalama” alisema Waziri Jafo.

Jumla ya Washiriki 44 kutoka Tanzania Bara na Visiwani wanatarajiwa kuhudhuria kozi hiyo inayotarajiwa kufungwa rasmi tarehe 02 Agosti 2019. Vilevile, Waziri Jafo aliutaka uongozi wa Jeshi kuongeza idadi ya Washiriki kwenye kozi hiyo ili viongozi wengi waweze kupata nafasi ya kushiriki Mafunzo hayo muhimu kwa Taifa.

Naye Mkuu wa Chuo hicho Luteni Jenerali Paul Massao alimhakikishia Waziri Jafo kuwa Chuo kitaendelea kutoa Mafunzo kwa Viongozi ili Taifa liendelee kuwa Salama na kuwa na Viongozi mahili ambao watalipeleka Taifa katika kufikia Uchumi wa Kati.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.