• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri Tax azindua bomu la kufukuza Tembo.

Waziri Tax azindua bomu la kufukuza Tembo. Posted On: Monday, 13th May 2024

Waziri wa Ulinzi na JKT Mheshimiwa Dkt Stergomena Tax amezindua bomu baridi lenye uwezo mkubwa wa kutawanya makundi ya Tembo yanayovamia makazi ya watu wanaoishi karibu na hifadhi za Taifa na mapori ya akiba.

Mheshimiwa Dkt Tax amelishukuru Shirika la Mzinga kwa kutengeneza bomu hilo huku akilitaka Shirika hilo kuendeleza ubunifu ili kuweza kulisaidia Taifa katika kukuza teknolojia. Amesema kuwa bomu hilo litasaidia kupunguza madhara ya uvamizi wa tembo kwani halmashauri 81 zimekuwa zikisumbuliwa na Wanyama hao. Aidha Dkt Taxi amezitaka taasisi zitakazotumia mabomu hayo kuyatumiakwa kuzingatia miongozo ili yasije yakaleta athari kwa watumiaji.

Akitoa taarifa kwa Mheshimiwa Waziri, Meneja Mkuu wa Shirika la Mzinga, Brigedia Jenerali Seif Hamis amesema kuwa bomu lililofanyiwa utafiti na kutengenezwa na Shirika hilo liko katika aina mbili ambapo wametengeneza bomu linaloweza kulipuka likiwa angani na lipo linaloweza kulipuka baada ya kutua ardhini. BrigediaHamis ameongeza kuwa Shirika la Mzinga kwa kushirikiana na wadau wengine kama Taasisi ya Utafiti wa Wanyama Pori litaendelea na tafiti mbalimbali ili kuwezesha kutokomezwa kwa tatizo la tembo kuvamia makazi ya watu.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Vikosi Chini ya Makao Makuu ya Jeshi Meja, Jenerali Idd Nkambi ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuliwezesha Jeshi kupitia Mashirika yake kwa rasilimali fedha, vifaa na wataalam hivyo kulifanya JWTZ kutekeleza majukumu yake kwa weledi.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.