• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE

Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE Posted On: Monday, 15th February 2021

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh. Elias Kwandikwa ameipongeza Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa kusaidia wanawake wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wanaoshirikiulinzi wa amani.

Waziri Kwandikwa amesema hayo leo katika kituo cha ulinzi wa amani (PTC) jijini Dar es Salaam wakati akikabidhiwa vifaa hivyo na Balozi wa UAE Mh. KhalifaAbdulrahman

Amesema Wizara itaendelea kuwashirikisha wanawake katika mambo mbalimbali kama ilivyo katika sekta nyingine hivyo aliwataka wazazi kuendelea kuwaunga mkono watoto wao wa kike ili kulitumikia taifa.

Kwa upande wake Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Mh. Abdulrahman alisema msaada huu ni kutambua mchango wa wanawake katika ulinzi wa amani.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yacoub Mohamed alisema msaada huu utasaidia kuongeza nguvu katika mahitaji ya wanawake hao walinda amani ambayo wamekuwa wakipatiwa.

Kwa upande wake mwakilishi wa walinda amani wanawake Meja Justina Gessine alisema wanawake walinda amani hukabiliwa na changamoto za kimazingira kutokana na hali zao lakini anashukuru Jeshi na wadau wengine kusaidia kuziondoa na kufanikisha malengo yaliyokusudiwa.

Sherehe za kukabidhi msaada huo zilihudhuriwa na Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita Meja Jenerali Alfred Kapinga, Mwakilishi mkazi wa Umoja wa MataifaZlatan Milisic, Mkurugenzi wa Jenda kutoka wizara afya mboni mgaza na macocha tembele kutoka wizara mambo ya nje.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.