• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

ZOEZI "USHIRIKIANO IMARA 2022" LAFUNGWA RASMI.

ZOEZI  "USHIRIKIANO IMARA 2022"  LAFUNGWA RASMI. Posted On: Saturday, 11th June 2022

Zoezi lililoandaliwa kwa kushirikiana na Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki limefungwa rasmi tarehe 10 June, 2022 ambapo mgeni rasmi alikuwa Mhe. Rebecca Alitwala Kadaga Makamu wa Kwanza wa Waziri Mkuu wa Uganda na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kufungwa kwa zoezi hili kunafuatia kukamilika kwa mazoezi yaliyopangwa kufanywa kwa pamoja ya namna ya kushiriki Misheni na Oparesheni mbalimbali, kupambana na Ugaidi, Uharamia na Majanga mengine .

Aidha, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Stergomena Tax alihudhuria ufungaji wa zoezi hilo na kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alitoa salamu za pongezi kwa mwenyeji Uganda kufanya maandalizi na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kushiriki zoezi hilo.

Nae Mkuu wa Utumishi Jeshini Meja Jenerali Paulo Kisesa Simuli kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi alipokea zawadi ya Ushiriki wa Kikundi cha Vyombo vya Ulinzi na Usalama cha Tanzania mara baada ya kufungwa zoezi hilo.

Ikumbukwe kuwa mazoezi haya yalifunguliwa rasmi 03 June, 2022 na washiriki wakiwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda ikiwa ni mwenyeji, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rwanda, Burundi, Kenya, na Sudani Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilikuwa kama mtazamaji.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.