• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano Posted On: Friday, 16th May 2025

Kikao cha 40 cha Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Ulinzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kimehitimishwa rasmi tarehe 16 May, 2025 jijini Arusha, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujadili mambo mbalimbali ya kisera na mipango ya ushirikiano wa kijeshi baina ya nchi wanachama.

Kikao hicho kilichofanyika chini ya Uenyekiti wa Dkt.Patrick Mariru Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi wa Kenya ambaye alimwakilisha Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo.

Akizungumza wakati wa ufungaji wa kikao hicho Dkt. Patrick Mariru ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kwa mapokezi mazuri na ukarimu walioupata kutoka kwa Watanzania katika kipindi chote cha Kikao hicho.

Aidha, amezitaka nchi wanachama kupitia majeshi yake kuendeleza umoja, mshikamano na kuimarisha ushirikiano na mazoezi ya pamoja katika masuala ya Ulinzi ili kuifanya Jumuiya hiyo kuwa sehemu salama dhidi ya matishio ya kiusalama.

Viongozi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walihudhuria kwenye kikao hicho, akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Veronica Mueni Nduva. Kwa upande wa Tanzania, uliwakilishwa na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Luteni Jenerali Salum Othman kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stargomena Tax.

Jumla ya nchi wanachama idadi nane ambazo ni Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Kenya, Rwanda, Somalia, Sudan Kusini, Uganda na mwenyeji Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilishiriki.

Habari Mpya

  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea masaa 13
  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.