• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ kuendelea kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la Rwanda

JWTZ kuendelea kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la Rwanda Posted On: Tuesday, 11th May 2021

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limesema litaendelea kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la Rwanda ili kudumisha amani na ustawi wa maendeleo kwa nchi zote mbili.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo alipokutana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Rwanda, Jenerali Jean Bosco Kazura tarehe 10 Mei 2021 jijini Dar es Salaam.

Jenerali Mabeyo amesema nchi za Tanzania na Rwanda ni jirani na zinatakiwa kuendeleza ushirikiano uliopo ili kuilinda amani iliyopo kati ya nchi hizo kwani kwa kufanya hivyo kutachochea maendeleo na kukuza uchumi.

Naye Mkuu wa Majeshi ya Rwanda Jenerali Jean Kazura amelishukuru JWTZ kwa kuwa mfano wa kuigwa barani Afrika na hivyo kuahidi kuongeza ushirikiano katika nyanja za mafunzo, ikiwa ni pamoja na kubadilishana wakufunzi ngazi za Maafisa Wanafunzi, Ukamanda na Unadhimu na Rwanda kupewa nafasi ngazi ya Chuo cha Ulinzi wa Taifa (National Dafence College). Maeneo mengine ya ushirikiano ni pamoja na kubadilishana habari za kiutambuzi na manufaa ya pande zote.

Mbali na ushirikiano katika maeneo tajwa, Jenerali Kazura pia amesisitiza na kuahidi kuendelea kuienzi lugha adhimu ya Kiswahili kwenye Jeshi lake.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.