• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

WAHITIMU NDC WATAKIWA KUWA MABALOZI WA AMANI

 WAHITIMU NDC WATAKIWA KUWA MABALOZI WA AMANI Posted On: Monday, 29th July 2019

Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Tanzania ni miongoni mwa Vyuo bora Afrika na Duniani ambavyo vinatoa mafunzo ya Usalama na Stratejia ya Kitaifa na Kimataifa. Hivi karibuni Chuo kimefanya Mahafali ya Saba tangu kuanzishwa kwake mwaka 2012.

Mgeni rasmi katika Mahafali hayo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Jumla ya wahitimu 39 wakiwemo Maafisa wa ngazi za juu kutoka katika nchi kumi na moja ikiwemo Tanzania, Botswana, Burundi, China, Kenya, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Zambia pamoja na Zimbabwe. Kutoka nchini washiriki wa kozi hiyo walitoka kwenyeVyombo vya Ulinzi na Usalama, Serikalini na Taasisi nyingine za Serikali na wahitimu hao waliweza kutunukiwa Stashahada na Shahada ya Uzamili.

Aidha, Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia aliwataka wahitimu watakaporudi katika nchi zao kuweza kuzishauri Serikali na Majeshi ya nchi wanazotoka kusimamia suala la amani ili kuondoa migogoro mbalimbali iliyopo katika nchi zao, kwani wamepewa nyenzo zote za kwenda kufanya kazi na kusaidia Serikali zao kutunga sera zitakazosaidia kutunza amani, utulivu na usalama katika nchi zetu hasa Afrika.

Afrika kuna changamoto nyingi za usalama kwa hiyo wanategemewa wao na wenzao ambao wamepita chuo kama hiki katika kutoa ushauri nchini mwao juu ya nini kifanyike ili Bara la Afrika libaki kuwa salama.

Habari Mpya

  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea wiki 1
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    TANGAZO LA NAFASI ZA KUANDIKISHWA JESHINI

    tokea wiki 2
  • ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    ​Jenerali Mkunda Ahitimisha Mafunzo Askari Wapya

    tokea wiki 2
  • Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    Meja Jenerali Nkambi ateta na Ujumbe kutoka Jeshi la Uganda

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.