Masters of Science in Defence Analysis
Luteni Jenerali Yakubu Mohamed ni Mnadhimu Mkuu wa JWTZ wa 13 tangu alipoteuliwa tarehe 14 February 2018 na Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano, Dk. John Pombe Magufuli.
Luteni Jenerali Yakubu Mohamed alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tarehe 01 Januari 1982 na kuhudhuria kozi ya afisa mwanafunzi na kupata kamisheni tarehe 02 Septemba 1987 kuwa Luteni Usu.
Luteni Jenerali Yakubu Mohamed alihudhuria kozi mbalimbali za kijeshi ndani na nje ya nchi, baadhi ya nchi hizo ni Misri, Afrika Kusini, Marekani na Uingereza.
Luteni Jenerali Yakubu Mohamed katika kulitumikia Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania alishika nyadhifa mbalimbali ikiwemo Afisa Mnadhimu - Makao Makuu ya Jeshi, Afisa Mnadhimu - Ulinzi wa Amani UNMIS(Sudan), Afisa Mnadhimu Baraza la Usalama la Taifa, Mratibu Msaidizi Mkuu Baraza la Usalama la Taifa, Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa – Tanzania.
Luteni Jenerali Yakubu Mohamed ametunukiwa medali mbalimbali
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 9203 Dar es Salaam,
Street :Magore, Upanga
Fax : +255 22 2153432
Tel : +255 22 2150592- 4
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.