Posted On: Tuesday, 24th February 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan leo tarehe 24 Februari 2026 amefungua rasmi jengo la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa lililopo katika Kijiji cha Kikombo , Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Katika uzinduzi huo Mh Rais aliwataka Maafisa na Askari kuendelea kuviishi viapo vyao kwa Ustawi wa Ulinzi na usalama wa Taifa la Tanzania.
Amesisitiza kuwa Jengo lililozinduliwa liwe chachu ya mageuzi ya kifikra katika mstakabali wa maendeleo ya Ulinzi wa Taifa.
Naye Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda alimshukuru Mh Rais kwa kutenga mda wake kwaajili ya Uzinduzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa pamoja na kuruhusu utekelezaji wa ujenzi huo kwa kutoa fedha ili kukamilisha ujenzi huo.
Pia aliwashukuru Maafisa na Askari pamoja na taasisi za Umma ikiwemo, Tanesco, Duwasa, Tarura, Halmashauri ya Jiji Dodoma pamoja na makampuni yaliyo chini ya JWTZ ambayo ni SumaJKT na Ngome J&U kwa ushirikiano walioutoa kwa pamoja katika kutekeleza dhamira ya ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.