Posted On: Tuesday, 9th June 2026
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salum Haji Othman ameweka jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Kijiji cha burudani kilichopo katika Kambi ya Jeshi Kisarawe Mkoani Pwani leo tarehe 08 Juni 26.
Akizungumza na Maafisa na Askari wa Kikosi cha mawasiliano Kisarawe, Luteni Jenerali Othman amesema kuanzishwa kwa miradi hii kutasaidia kikosi kutatua changamoto za mbalimbalii.
Miradi iliyoanzishwa ni pamoja na Ujenzi wa uwanja wa michezo, maegesho ya magari ya mizigo, Ujenzi wa Ukumbi wa Burudani na Ujenzi wa kituo cha mafuta.
Aidha, Luteni Jenerali Othman amewataka wanakikosi kuepuka tabia zisizofaa ikiwemo matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi mabaya ya mitandao ya Kijamii, uraibu wa kushiriki michezo ya kubashiri na ulevi uliokithiri.
Pia, wanakikosi wametakiwa kuyaishi maneno manne kwa mwanajeshi ikiwemo nidhamu nzuri, Utii, Uhodari na Uaminifu, maneno ambayo hayana budi kuzingatiwa wakati wote.
Naye, Kamanda Kikosi cha mawasiliano Kisarawe Kanali Mwakisamba amemshukuru Mnadhimu Mkuu Luteni Jenerali Salum Haji Othman kwa kuweka jiwe la msingi kujengwa kwa miradi ya kikosi, na kuahidi kukamilisha miradi hiyo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na maafisa Jenerali na Wakuu wa Vikosi kutoka Kanda ya Pwani na Dar es Salaam pamoja na Wanakikosi.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.