• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

BAMMATA kutimua vumbi tarehe 23 Uwanja wa Uhuru

BAMMATA  kutimua vumbi  tarehe 23 Uwanja wa Uhuru Posted On: Thursday, 21st February 2019

Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA), limesema kuwa michezo ya majeshi Tanzania itaanza kutimua vumbi tarehe 23 mwezi huu katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Upanga jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Baraza hilo Brigedia Jenerali Suleiman Mzee amesema kuwa jumla ya Kanda saba zitashiriki katika Michezo hiyo.

Kwa mwaka huu michezo ya BAMMATA inashirikisha kanda saba (7) ambapo timuza michezo mbalimbali zinatoka ndani ya kanda hizo. Kanda zinazoshiriki mwaka huu ni Ngome, JKT, Polisi, Magereza, SMZ (Idara Maalumu), Uhamiaji, Zimamoto na Uokoaji.

  • Mashindano hayo yatashirikisha mchezo wa mpira wa miguu (Football) wanaume, mpira wa mikono (Handball) wanaume na wanawake, mpira wa wavu (Volleyball) wanaume na wanawake, mpira wa kikapu (Basketball) wanaume na wanawake, ndondi wanaume na ulengaji shabaha wanaume na Wanawake.
  • Lengo la mashindano hayo ni kuibua na kukuza vipaji, kuendeleza elimu ya viungo na utimamu wa mwili, kuendeleza uhusiano, urafiki na udugu baina ya Majeshi ya Ulinzi, Usalama na Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wananchi kwa ujumla.
  • Pamoja na malengo hayo pia kushirikiana na mabaraza ya michezo ya Taifa na mashirikisho ya michezo ya kitaifa na kimataifa ili kuendeleza michezo katika Majeshi, kuendeleza na kudumisha sera ya Taifa kuimarisha timu zilizomo ndani ya kanda za BAMMATA.
  • Mgeni rasmi katika ufunguzi huo ni Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Idd. Michezo ya BAMMATA ilianza rasmi mwaka 1977 na kuendelea kufanyika mpaka hivi sasa.

Habari Mpya

  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 2
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea wiki 3
  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea mwezi 1
  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.