• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Dr Nyamsaho atembelea Makao Makuu ya Jeshi

Dr Nyamsaho atembelea Makao Makuu ya Jeshi Posted On: Friday, 5th December 2025

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Dkt Rhimo Nyamsaho amefanya ziara fupi Makao Makuu ya Jeshi Msalato Dodoma leo tarehe 05 Desemba 2025 kwa lengo la kujitambulisha.

Baada kupokelewa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda, Dkt Rhimo Nyamsaho alizungumza na Maafisa na Askari akiwaasa kudumisha umoja na mshikamano katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Alisisitiza suala zima la kutanguliza maslahi ya Taifa ili kuhakikisha suala la Ulinzi wa Taifa linaimarika kwa kiwango cha juu.

Mhe. Waziri aliwataka Maafisa na Askari kudumisha sifa ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tangu kuasisiwa kwake kwa kuendelea kuviishi viapo vyao ikiwemo Nidhamu nzuri, Utii, Uhodari na Uaminifu.

Kwa upande wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amempongeza Mheshimiwa Dkt Nyamsaho kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi na JKT na kumuhakikishia kuwa JWTZ liko imara na tayari wakati wote kutekeleza majukumu yake kwa nidhamu na uadilifu wa hali ya juu.

Habari Mpya

  • Dr Nyamsaho atembelea Makao Makuu ya Jeshi

    Dr Nyamsaho atembelea Makao Makuu ya Jeshi

    tokea masaa 4
  • Rais Samia atunuku Kamisheni

    Rais Samia atunuku Kamisheni

    tokea wiki 1
  • Rais Samia ala Kiapo

    Rais Samia ala Kiapo

    tokea mwezi 1
  • JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon

    JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 9
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 9
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 9
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 3
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.