• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Jenerali Venance Mabeyo akutana na Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma

Jenerali Venance Mabeyo akutana na Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma Posted On: Thursday, 24th January 2019

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo leo amekutana na Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wanaofanya kazi katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani katika kikao kilichofanyika kwenye viwanja vya Lugalo Jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho Mkuu wa Majeshi alitoa salam za mwaka mpya na kuwashukuru Maafisa na Askari kwa kufanya kazi kwa weledi, kwa mafanikio makubwa yaliopatikana mwaka jana na kusisitiza kuyaendeleza mafanikio hayo ili mwaka 2019 uwe wa mafanikio zaidi.

Vilevile aliwakumbusha Maafisa na Askari kuendeleza na kuudumisha ushirikiano mzuri kwa ngazi zote baina ya JWTZ na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama. Alisema mshikamano ndio dira ya kuletaupendo na kutambua majukumu ambayo tunapaswa kuyatekeleza kulingana na kiapo chetu kwa lengo la kulitumikia Taifa.

“Wajibu wa kwanza wa mwanajeshi ni kulinda mipaka ya nchi, watu pamoja na mali zao” alisema Jenerali Mabeyo. Aidha, aliwataka Maafisa na Askari kuwa wa kwanza katika kuwalinda wananchi kwani Wanajeshi ni tegemeo la wananchi kiulinzi.

Pia aliwataka Maafisa na Askari kutii na kuthamini kiapo chao na kuweka uzalendo mbele ili kuwezakufanya kazi kwa ufanisi. “Changamoto tulizozipata mwaka jana katika kutekeleza majukumu yetu tuzigeuze kuwa fursa kwa mwaka huu wa 2019” alisema Jenerali VenanceMabeyo.

Habari Mpya

  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 2
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea wiki 3
  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea mwezi 1
  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.