• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon

JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon Posted On: Friday, 24th October 2025

Kikundi cha Polisi Jeshi cha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kinachohudumu kwenye Ulinzi wa Amani nchini Lebanon chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa (UNIFIL) leo tarehe 24 Oktoba, 2025 kimejumuika na Mataifa mengine yanayoshiriki katika Ulinzi wa Amani nchini humo katika kuadhimisha Siku ya Umoja wa Mataifa (UN DAY) .

Maadhimisho hayo yamefanyika kwa gwaride maalumu lililoandaliwa na vikundi kutoka mataifa yanayoshiriki kwenye jukumu la Ulinzi wa Amani nchini humo.

Siku ya Umoja wa Mataifa huadhimishwa kila ifikapo tarehe 24 Oktoba ikiwa ni kumbukizi ya kuanzishwa kwa Umoja huo ambao ulianzishwa rasmi mwaka 1945.

Leo hii vikundi hivyo vinapoadhimisha Siku hiyo, Umoja huo unatimiza miaka 80 toka kuundwa kwake.

Vikundi vyetu vya Polisi Jeshi vimekuwa vikiliwakilisha vema Jeshi letu kwa kutekeleza majukumu yake kwa nidhamu, utiifu, uhodari, uaminifu na weledi wa hali ya juu na hivyo kuendelea kuliletea sifa nzuri Jeshi letu na Taifa kwa ujumla katika anga za Kimataifa.

Kutokana na sifa nzuri ambazo Jeshi limekuwa likijizolea kutokana na utekelezaji wake wa majukumu, Tanzania imeendelea kuaminiwa na kushiriki katika majukumu ya Ulinzi wa Amani katika nchi mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR), Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Msumbiji.

Habari Mpya

  • JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon

    JWTZ Laadhimisha UN DAY Lebanon

    tokea masaa 12
  • Jeshi kujenga Hoteli ya nyota tano

    Jeshi kujenga Hoteli ya nyota tano

    tokea wiki 2
  • Tanzania kuanzisha Kiwanda cha Magari

    Tanzania kuanzisha Kiwanda cha Magari

    tokea wiki 3
  • Amiri Jeshi Mkuu amzawadia Nyumba Simbu

    Amiri Jeshi Mkuu amzawadia Nyumba Simbu

    tokea wiki 3
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 9
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 9
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 3
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.