Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewaaga Majenerali wake 9 baada ya kustaafu rasmi kwa heshima kwa kutimiza umri wa lazima wa kustaafu utumishi Jeshini.
Majenerali hao wastaafu wameagwa kwa Gwaride rasmi lililofanyika katika viwanja vya Kambi ya Jeshi ya Jenerali Abadallah Twalipo iliyopo Mgulani jijini Dar es Salaam.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania pamoja na baadhi ya viongozi wengine waliostaafu Jeshini kwa kipindi cha nyuma, akiwemo aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi Luteni Jenerali James Mwakibirwa.
Aidha, baada ya hapo, walisindikizwa na gwaride lililoandaliwa rasmi kwa ajili yao, huku wakisukumwa kwenye Magari kama tendo la kuashiria kuwasindikiza kwa kuwa wamemaliza utumishi wao kwa heshima na salama.
Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz
Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.