• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Mafunzo Ya Ngumi Na Mpira Wa Kikapu Yafungwa Rasmi

Mafunzo Ya Ngumi Na Mpira Wa Kikapu Yafungwa Rasmi Posted On: Friday, 2nd November 2018

Mafunzo ya Makocha wa mchezo wa Ngumi na Mpira wa Kikapu yaliyokuwa yakiendeshwa kwa Makocha wa JWTZ yamefungwa rasmi tarehe 01 Februari 2018 kwenye Kambi ya JKT Mgulani.

Mafunzo hayo yalijumuisha Makocha wa michezo hiyo kutoka sehemu mbalimbali ikiwemo JWTZ, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na wengine kutoka Taasisi mbalimbali.

Akifunga mafunzo hayo mgeni rasmi Brigedia Jenerali Suleimani Mzee amewataka wahitimu hao kwenda kukifanyia kazi kile ambacho wamejifunza katika kipindi chote cha wiki mbili ili kuweza kuibua na kukuza vipaji vya Wanamichezo wetu.

Naye Mkufunzi kutoka Ujerumani Kapteni Paul Klar ameushukuru uongozi wa Jeshi na Washiriki kwa kuonesha ushirikiano wa karibu kwa kipindi chote cha mafunzo na kusema wana imani mafunzo hayo yatazaa matunda mema.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Wahitimu wenzake mwakilishi wa wahitimu hao Meja Kelvin Byabato ameushukuru uongozi wa Jeshi kupitia Ubalozi wa Tanzania na Mwakilishi wa Jeshi katika Baraza la Michezo ya Kijeshi Duniani (CISM),Kanali Joseph Bakar, kuwa kitendo cha kuwaleta wakufunzi hao kitawaongezea ujuzi na mbinu mpya katika michezo hiyo na hivyo kuzifanya timu za Jeshi na ya Taifa kuwa na watu wenye sifa na kuliletea sifa Taifa letu.

Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi tarehe 22 Oktoba 2018 na kufungwa tarehe 01 Novemba 2018.

Habari Mpya

  • ​Tanzania yatiliana saini na Serikali ya Ujerumani

    ​Tanzania yatiliana saini na Serikali ya Ujerumani

    tokea wiki 1
  • Jenerali Venance Mabeyo afanya ziara Shinyanga

    Jenerali Venance Mabeyo afanya ziara Shinyanga

    tokea wiki 1
  • Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE

    Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE

    tokea wiki 1
  • TANZIA

    TANZIA

    tokea wiki 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 4
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 4
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 4
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 4
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 9203 Dar es Salaam,
Street :Magore, Upanga
Fax : +255 22 2153432
Tel : +255 22 2150592- 4
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.