• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Mashindano ya BAMMATA yazinduliwa

Mashindano ya BAMMATA yazinduliwa Posted On: Sunday, 7th September 2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezindua Mashindano ya Michezo ya Majeshi BAMMATA kwa mwaka wa 2025, ambayo yanafanyika mjini Zanzibar.

Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya Mao Zedong na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mawaziri, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na wananchi.

Akitoa hotuba yake, Dkt Mwinyi amewataka washiriki wote wa mashindano hayo kutambua kuwa michezo ni kielelezo cha mshikamano wa kitaifa baina ya vyombo vyote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha Dkt. Mwinyi amesema "Serikali itaendelea kuunga mkono sekta ya michezo ili kukuza vipaji kwa vijana wa kitanzania sambamba na kuzijengea uwezo timu za majeshi ziweze kufanya vizuri kimataifa".

Mwisho aliwataka wachezaji wote wanaoshiriki michuano ya BAMMATA kucheza kwa nidhamu, utiifu na uhodari kama msingi wa Majeshi yote ulivyo ili kuleta burudani ya mashindano.

Nae Waziri wa Michezo wa Zanzibar Mhe. Tabia Mwita amempongeza Rais wa Zanzibar kwa ushirikiano anautoa katika sekta ya michezo ambapo mafanikio yaliyopatikana hadi sasa ni pamoja na ukarabati wa viwanja vya Amani Maisala na Gombani Pemba

Kwa upande wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali John Mkunda ameishukuru Serikali ya Zanzibar kupitia Wizara ya Michezo kwa kukubali mashindano hayo kufanyika Visiwani humo.

Amesema lengo mojawapo la mashindano hayo ni "vitalu vya kukuza na kuibua vipaji."

Nae Mwenyekiti wa BAMMATA Brigedia Jenerali Said Hamis akitoa utangulizi, ameainisha viwanja vitakavyotumika ambavyo ni Amani Complex mchezo wa riadha, na viwanja vya Maisala na Mao Zedong ambapo michezo mbalimbali itachezwa.

Ameitaja michezo hiyo kuwa ni Mpira wa Pete wanawake, mpira wa miguu wanaume, mpira wa kikapu wanaume na wanawake, riadha wanawake na wanaume na shabaha kwa jinsia zote na mpira wa wavu.

Mashindano hayo ambayo yataanza kutimua vumbi kesho, yatahusisha Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama upande wa bara na visiwani kwa michezo mbalimbali

Habari Mpya

  • Mashindano ya BAMMATA yazinduliwa

    Mashindano ya BAMMATA yazinduliwa

    tokea siku 2
  • Mkuu wa Majeshi ya UAE afanya Ziara Tanzania

    Mkuu wa Majeshi ya UAE afanya Ziara Tanzania

    tokea mwezi 1
  • JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    JWTZ latoa msaada kwa Manusura wa mauaji ya Kimbari Nchini Rwanda

    tokea miezi 2
  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa afungua mashindano ya CDF CUP.

    tokea miezi 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.