• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

NAFASI ZA KUJIUNGA NA JESHI

NAFASI ZA KUJIUNGA NA JESHI Posted On: Thursday, 9th March 2023

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA

NAFASI ZA KUJIUNGA NA JESHI

1.Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linatangaza nafasi za kujiunga na Jeshi kwa Vijana wa Kitanzania wenye elimu ya kuanzia Kidato cha Nne hadi Shahada ya Uzamili ambao wamemaliza Mkataba wa Mafunzo ya Kujitolea JKT na kurudishwa majumbani.

SIFA ZA MWOMBAJI

2.Vijana wa Kitanzania wenye nia ya kuandikishwa Jeshi wanatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-

a.Awe raia wa Tanzania wa kuzaliwa mwenye Kitambulisho cha Taifa.

b.Awe na umri wa miaka 18 hadi 26 kwa wenye elimu ya Kidato cha Nne hadi Kidato cha Sita na umri usiozidi miaka 27 kwa wenye elimu ya Juu.

c.Awe na afya nzuri na akili timamu.

d.Awe Mtanzania mwenye tabia na nidhamu nzuri, hajapatikana na hatia ya makosa ya jinai Mahakamani na kufungwa.

e.Awe na cheti halisi cha kuzaliwa (Original Birth Certificate), vyeti vya Shule na vyeti vya Taaluma.

f.Awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza, Chuo cha Mafunzo au Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM).

g.Asiwe ameoa au kuolewa.

h.Awe amehitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mkataba wa kujitolea miaka miwili (2) na kutunukiwa cheti. Wale vijana wa JKT waliopo Makambini ambao wana sifa tayari, utaratibu wao wa kuwaandikisha unafanyika tofauti na vijana waliopo majumbani ambao tangazo hili linawahusu.

UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI

3.Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yawasilishwe Makao Makuu ya Jeshi Dodoma kuanzia tarehe ya tangazo hili hadi tarehe 20 Machi, 2023 yakiwa na viambatisho vifuatavyo:-

a.Nakala ya Kitambulisho cha Taifa au namba ya NIDA.

b.Nakala ya cheti cha kuzaliwa, vyeti vya Shule na Chuo.

c.Nakala ya cheti cha JKT.

d.Namba ya simu ya mkononi ya mwombaji.

MAOMBI YATUMWE KWA ANUANI IFUATAVYO

4.a.Mkuu wa Utumishi,

Makao Makuu ya Jeshi,

Sanduku la Posta 194,

DODOMA, Tanzania.

b.Email: ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Description: C:\Users\PS DIPR\AppData\Local\Microsoft\Windows\INetCache\Content.Word\IMG-20230309-WA0007.jpg

Habari Mpya

  • NAFASI ZA KUJIUNGA NA JESHI

    NAFASI ZA KUJIUNGA NA JESHI

    tokea wiki 2
  • Rais Samia Suluhu Hassan atunuku Kamisheni

    Rais Samia Suluhu Hassan atunuku Kamisheni

    tokea miezi 3
  • Waziri Mhe. Bashungwa atembelea zoezi Dragon Fly

    Waziri Mhe. Bashungwa atembelea zoezi Dragon Fly

    tokea miezi 4
  • Zoezi Dragon Fly lafunguliwa

    Zoezi Dragon Fly lafunguliwa

    tokea miezi 5
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 6
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 6
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 6
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miezi 6
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.