• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Rais Dkt. John Magufuli atunuku Kamisheni

Rais Dkt. John  Magufuli atunuku Kamisheni Posted On: Saturday, 30th March 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Magufuli leo tarehe 30 Machi 2019 amewatunuku Kamisheni Maafisa wapya 146 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Maafisa hao wametunukiwa cheo cha Luteni Usu baada ya kumaliza mafunzo yao katika Chuo cha Maafisa Wanafunzi kilichopo Monduli Jijini Arusha. Miongoni mwa maafisa waliotunukiwa kamisheni leo 140 ni wanaume na sita (6) ni Wanawake.

Rais Magufuli alisema kuwa Jeshi limekuwa likifanya vizuri katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Kitaifa na kimataifa na kuiletea sifa nzuri nchi yetu.

Aidha, aliendelea kuwapongeza Maafisa hao wapya kwa kuweza kufanya vizuri na kuonesha nidhamu nzuri kwa wakuu wao katika kipindi chote cha mafunzo licha ya kupitia katika mazingira magumu ya mafunzo ya kivita.

Naye Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Venance Mabeyo amewaasa Maafisa waliotunukiwa kamisheni kuheshimu kiapo chao na kufanya kazi kwa uadilifu wakitanguliza uzalendo na utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maafisa waliotunukiwa kamisheni wanazo taaluma mbalimbali katika viwango tofauti vya elimu ikiwa ni pamoja na Shahada ya Uzamili, Shahada ya kwanza, Stashahada ya Juu na Stashahada.

Habari Mpya

  • Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    Luteni Jenerali Othman ashiriki Kongamano kuhusu Usalama wa Kitaifa

    tokea wiki 2
  • Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    Jenerali Mkunda afungua Kikao cha Wakuu wa Majeshi SADC

    tokea wiki 3
  • Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha  Ushirikiano

    Afrika Mashariki Yaendelea Kuimarisha Ushirikiano

    tokea mwezi 1
  • ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    ​Jenerali Mkunda aweka Jiwe la Msingi Mradi wa Kokoto Arusha

    tokea mwezi 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 8
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 2
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.