• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
    • Kamandi ya Jeshi la Akiba
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Sajini Simbu apokelewa Kishujaa

Sajini Simbu apokelewa Kishujaa Posted On: Wednesday, 24th September 2025

Mshindi wa medali ya dhahabu katika Mashindano ya Marathoni ya Dunia yaliyofanyika Tokyo Japan Sajini Alphonce Simbu amepokelewa kishujaa na Serikali kwa kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jijini Dar es Salaam.

Akiongea mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Michezo Jeshini Luteni Kanali Penina Igwe amesema Sajini Simbu amekuwa shujaa wa Taifa letu la Tanzania kwa kutuletea medali ya dhahabu kwa kuwa medali hii ni ya kwanza katika nchi yetu hivyo anastahili pongezi.

Luteni Kanali Igwe aliongeza kuwa, Simbu ameliheshimisha taifa kwa ujumla na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa kuleta medali ya dhahabu hapa nchini.

"Hongera sana Simbu kwa kazi nzuri uliyoifanya, leo hii Taifa na Wanamichezo wenzako wamekuja kukupokea kwa heshima kubwa hivyo tunakuombea ufanikiwe zaidi na zaidi," alisema Igwe.

Kwa upande wake Sajini Simbu, ameishukuru Serikali, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania na Watanzania kumuwezesha kupata medali na kuipatia heshima Tanzania.

"Mafunzo mazuri niliyoyapata kutoka kwa kocha wangu tukiwa Jijini Arusha na malezi mazuri ya JWTZ ndio leo vimechangia kutwaa ubingwa wa Marathoni ya Dunia" alisema Simbu.

Sajini Simbu alilakiwa na mke wake Rehema Daudi Ngimba na mama yake mzazi Salome Mbua.

Habari Mpya

  • Tanzania kuanzisha Kiwanda cha Magari

    Tanzania kuanzisha Kiwanda cha Magari

    tokea siku 3
  • Amiri Jeshi Mkuu amzawadia Nyumba Simbu

    Amiri Jeshi Mkuu amzawadia Nyumba Simbu

    tokea siku 5
  • Sajini Simbu apokelewa Kishujaa

    Sajini Simbu apokelewa Kishujaa

    tokea wiki 1
  • Ngome yazidi kung'ara BAMMATA

    Ngome yazidi kung'ara BAMMATA

    tokea wiki 2
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 9
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 8
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 8
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 3
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 194 Dodoma,
Street : Miyuji, Msalato
Fax : +255 26 2962123
Tel : +255 737 962 064
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.