• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • Kiswahili
  • English

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania

  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira,Dhima na Majukumu
  • Kujiunga na JWTZ
  • Kamandi
    • Kamandi ya Jeshi la Wanamaji
    • Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu
    • Kamandi ya Jeshi la Anga
    • Jeshi la Kujenga Taifa
    • Kamandi ya Makao Makuu ya Jeshi
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Michezo
    • Viwanda
  • Oparesheni
    • Endelevu
    • Iliyokamilika
  • Kumbukumbu
    • Video
    • Picha
    • Hotuba

Tanzania yailaza Burundi 7-3

Tanzania yailaza Burundi 7-3 Posted On: Monday, 19th August 2019

Timu ya Mpira wa Miguu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) imefanikiwa kuilaza Timu ya Jeshi la Burundi Muzinga FCkwa ushindi mabao 7-0 mchezo wake wa kwanza katika Mashindano ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki yanayoendelea nchini Kenya.

Katika mchezo ulionza majira ya saa tisa jioni Tanzania ilikuwa ya kwanza kufumania nyavu za Burundikatika dakika ya nane ya mchezo kupitia kwa Mshambuliaji wake Samweli Kamuntu.

Baada ya bao hilo Tanzania iliendelea kulishambulia lango la Muzinga FC na kufanikiwa kuongeza goli la pilikatika dakika (34) kupitia kwa Mshambulia wake Fuluzulu Maganga ambaye alionekana kuwa mwiba kwa Burundi.

Mnamo dakika ya (45) Tanzania iliongeza goli la tatu kupitia kwa winga wake Anwary Kilemile aliyewatoka mabeki wa Burundi na kuachia mkwaju mkali uliomshinda mlinda mlango wa Burundi na kutinga wavuni.

Kipindi cha pili Burundi waliweza kupata goli la kwanza katika ( 47 ) na dakika tatu baadae(50) waliongeza goli la pili.

Hali hiyo iliwaamshawachezaji wa Timu ya Tanzania na kuanza kulishambulia lango la Timu ya Muzinga FC. Mashambulizihayo yaliweza kuzaa matunda kwakuongeza goli la nne kupitia kwa Edward Songo lililopatikana katika dakika (54).

Fuluzulu Maganga tena aliweza kuipatia Tanzania bao la Tano katika dakika (63) na kukamilisha mabao matatu aliyoyafunga kwenye mchezo huo na kuondoka na mpira. Dakika saba baadae Burundi walijipatia goli la tatu.

Dakika (86) Edward Songo tena aliinua Tanzania kwa kufunga goli la Saba, na hivyo kufanya Tanzania kutoka uwanjani kifua mbele kwa magoli 7-3.

Habari Mpya

  • ​Tanzania yatiliana saini na Serikali ya Ujerumani

    ​Tanzania yatiliana saini na Serikali ya Ujerumani

    tokea wiki 1
  • Jenerali Venance Mabeyo afanya ziara Shinyanga

    Jenerali Venance Mabeyo afanya ziara Shinyanga

    tokea wiki 1
  • Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE

    Waziri wa Ulinzi na JKT aipongeza Serikali ya UAE

    tokea wiki 1
  • TANZIA

    TANZIA

    tokea wiki 1
  • Zaidi

Nifanyeje

  • Utaratibu wa kujiunga na JWTZ tokea miaka 4
  • Majukumu ya Msingi ya JWTZ tokea miaka 4
  • Wakuu wa Majeshi waliopita JWTZ tokea miaka 4
  • Wanadhimu Wakuu waliopita JWTZ tokea miaka 4
  • Zaidi

Wasiliana Nasi

Tanzania People's Defence Forces,
P.O.Box 9203 Dar es Salaam,
Street :Magore, Upanga
Fax : +255 22 2153432
Tel : +255 22 2150592- 4
E-mail : ulinzimagazine@tpdf.mil.tz

Kurasa za Karibu

  • Marais walioongoza Tanzania
  • Tangazo kwa vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria 2016
  • Taarifa kuhusu vijana kujiunga na JKT

Tovuti Mashuhuri

  • Shirika la Uzalishaji Mali - SUMAJKT
  • Tovuti ya Ikulu
  • Jeshi la Kujenga Taifa
  • Wizara ya Ulinzi na Kujenga Taifa
  • Chuo cha Ulinzi wa Taifa - Tanzania

Jarida la Ulinzi

Zaidi

Haki zote zimehifadhiwa. Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.